
NA DANIEL LIMBE
Askari wa Hifadhi ya Kisiwa cha Rubondo wilayani
Geita mkoani hapa, wamekumbwa na kashfa nyingine
baada ya kudaiwa kumuua raia mmoja kwa kipigo
mbele ya kituo kidogo cha polisi Chato.
Aliyeuawa ametambulika kuwa ni Moshi Nkola
(39), mkazi wa kijiji cha Mkuyuni kata ya
Chato wilayani hapa.
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Geita, Pudensiana Protas,
alidai kutokuwa na taarifa ya tukio hilo na kuahidi kufuatilia
ukweli wa jambo hilo kutoka kwa wasaidizi wake.
Akielezea tukio hilo, kaka wa marehemu, Paulo Nkola (42),
aliliambia NIPASHE Jumapili kuwa nduguye alipigwa na
askari wawili wa hifadhi ya kisiw
a cha Rubondo (hakuwataja majina) Oktoba 17, majira
ya saa 4 usiku wakati akitoka kwenye duka la kuuza pombe.
Alisema
kabla ya kipigo hicho, Nkola alikuwa akiendesha
pikipiki yake wakati akirejea nyumbani kwake na baadaye
alikutana na askari hao wakamtaka awabebe kwenye pikipiki
hiyo kwa nguvu kwa lengo la kuwapeleka kwenye mwalo wa
kasenda ambapo kuna ghati la kuvukia ili kuingia ndani ya
hifadhi hiyo.
Baada ya kukaidi amri ya askari hao, mmoja wao alipanda
kwa makusudi wakati Nkola akitaka kuondoka eneo hilo,
hali iliyosababisha kuyumba na kuanguka. Kitendo hicho
kilichowaudhi askari hao na kuanza kumshambulia kwa kipigo.
Paulo alisema baada ya mdogo wake kuzidiwa nguvu, alilazimika
kukimbilia kituo kidogo cha polisi cha Muganza ili kunusuru
maisha yake, lakini katika hali isiyokuwa ya kawaida watu hao
walimfuata mpaka kituoni hapo na kuendelea kumpiga mbele ya
askari wa polisi waliokuwa zamu.
Kutokana na kipigo hicho, Nkola alijeruhiwa vibaya na baadaye
kuomba PF3 kwa ajili ya matibabu kwenye zahanati ya
Nyabugera iliyopo kata ya Muganza.
Hata hivyo, baada ya hali ya Nkola kuonekana kuzidi kuwa
mbaya, alilazimika kwenda hospitali ya wilaya ya Chato ili
kupata huduma zaidi kabla ya kukumbwa na mauti hayo
usiku wa kuamkia jana.
Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo, Mashaka Majige, maarufu
kwa jina la Kishimba, alisema askari hao pia walikuwa wamelewa
pombe ambapo walimtaka Moshi awabebe kwenye pikipiki kwa
nguvu ambapo alikaidi amri hiyo.
Alisema hata baada ya merehemu kukimbilia kituo cha polisi na
kuingia ndani, askari hao walimfuata na kumshambulia mbele
ya askari waliokuwepo bila kuwazuia.
Diwani wa kata ya Muganza, Marco Maduka, amekiri kutokea
tukio hilo na kudai kuwa askari hao walikuwa wametoka kwenye
hifadhi ya kisiwa cha Rubondo na kwamba walionekana wakinywa
pombe kabla ya kufanya ukatili huo.
Alidai kuwa askari hao ambao majina yao hayajafahamika mara
moja, walimpiga mtu huyo ndani ya kituo cha polisi kabla ya
kukumbwa na mauti.
Jeshi la polisi wilayani hapa limekiri kuwapo kwa madai hayo
na uchunguzi unafanyika. Hakuna aliyekamatwa kuhusiana na
mauaji hayo.
NIPASHE Jumapili lilipomtafuta Ofisa doria mkuu wa hifadhi ya
kisiwa cha Rubondo, aliyefahamika kwa jina moja la Chuwa ili
kuzungumzia tuhuma hizo simu yake haikupatikana.
Mganga mkuu wa hospitali ya Wilaya ya Chato, Dk. Pius Buchukundi,
alikiri kupokelewa kwa Nkola akiwa mgonjwa lakini wakati akipatiwa
matibabu alipoteza maisha.
Uchunguzi wa kitabibu umebaini kuwa Nkola aliumia kichwa
kutokana na kitu kisichojulikana kumgonga na kusababisha kupasuka
baadhi ya mishipa iliyosababisha damu nyingi kuvuja eneo la jicho.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
pikipiki yake wakati akirejea nyumbani kwake na baadaye
alikutana na askari hao wakamtaka awabebe kwenye pikipiki
hiyo kwa nguvu kwa lengo la kuwapeleka kwenye mwalo wa
kasenda ambapo kuna ghati la kuvukia ili kuingia ndani ya
hifadhi hiyo.
Baada ya kukaidi amri ya askari hao, mmoja wao alipanda
kwa makusudi wakati Nkola akitaka kuondoka eneo hilo,
hali iliyosababisha kuyumba na kuanguka. Kitendo hicho
kilichowaudhi askari hao na kuanza kumshambulia kwa kipigo.
Paulo alisema baada ya mdogo wake kuzidiwa nguvu, alilazimika
kukimbilia kituo kidogo cha polisi cha Muganza ili kunusuru
maisha yake, lakini katika hali isiyokuwa ya kawaida watu hao
walimfuata mpaka kituoni hapo na kuendelea kumpiga mbele ya
askari wa polisi waliokuwa zamu.
Kutokana na kipigo hicho, Nkola alijeruhiwa vibaya na baadaye
kuomba PF3 kwa ajili ya matibabu kwenye zahanati ya
Nyabugera iliyopo kata ya Muganza.
Hata hivyo, baada ya hali ya Nkola kuonekana kuzidi kuwa
mbaya, alilazimika kwenda hospitali ya wilaya ya Chato ili
kupata huduma zaidi kabla ya kukumbwa na mauti hayo
usiku wa kuamkia jana.
Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo, Mashaka Majige, maarufu
kwa jina la Kishimba, alisema askari hao pia walikuwa wamelewa
pombe ambapo walimtaka Moshi awabebe kwenye pikipiki kwa
nguvu ambapo alikaidi amri hiyo.
Alisema hata baada ya merehemu kukimbilia kituo cha polisi na
kuingia ndani, askari hao walimfuata na kumshambulia mbele
ya askari waliokuwepo bila kuwazuia.
Diwani wa kata ya Muganza, Marco Maduka, amekiri kutokea
tukio hilo na kudai kuwa askari hao walikuwa wametoka kwenye
hifadhi ya kisiwa cha Rubondo na kwamba walionekana wakinywa
pombe kabla ya kufanya ukatili huo.
Alidai kuwa askari hao ambao majina yao hayajafahamika mara
moja, walimpiga mtu huyo ndani ya kituo cha polisi kabla ya
kukumbwa na mauti.
Jeshi la polisi wilayani hapa limekiri kuwapo kwa madai hayo
na uchunguzi unafanyika. Hakuna aliyekamatwa kuhusiana na
mauaji hayo.
NIPASHE Jumapili lilipomtafuta Ofisa doria mkuu wa hifadhi ya
kisiwa cha Rubondo, aliyefahamika kwa jina moja la Chuwa ili
kuzungumzia tuhuma hizo simu yake haikupatikana.
Mganga mkuu wa hospitali ya Wilaya ya Chato, Dk. Pius Buchukundi,
alikiri kupokelewa kwa Nkola akiwa mgonjwa lakini wakati akipatiwa
matibabu alipoteza maisha.
Uchunguzi wa kitabibu umebaini kuwa Nkola aliumia kichwa
kutokana na kitu kisichojulikana kumgonga na kusababisha kupasuka
baadhi ya mishipa iliyosababisha damu nyingi kuvuja eneo la jicho.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
No comments:
Post a Comment