Watu 36 wamefariki dunia papohapo na wengine 79 kujerihiwa vibaya
katika ajali mbaya ambayo imetokea saa tano leo asbuhi katika kijiji
cha sabasaba nje kidogo ya mji wa musoma wilaya ya butiama mkoani
mara kwa kuhusisha mabasi mawili ya abiria na gari dogo aina ya Nissani
Tellono yenye namba za usajili T332 AKK.
Mbali na gari hilo kugongwa na kutumbukia ndani ya
mto mmoja katika daraja hilo kwenye barabara kuu ya Musoma –Mwanza pia
mabasi mawili ambayo yamehusika katika ajali mbaya ni j4
express yenye namba za usali T677 CYC liyokuwa ikitokea jijini Mwanza
kwenda sirari wilayani tarime ambalo limegongano uso kwa uso na
basi la Mwanza coach yenye namba T736 AWJ lilokuwa likitokea Musoma
kwenda jijini Mwanza.
Baada ya taarifa za ajali kusambaa katika manipaa
ya musoma vilio na simanzi vimetawala katika mji huo wa Musoma
mkoani Mara baada majeruhi na miili ya marehemu wa ajali hiyo
kuanza kufikishwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mara mjini
Musoma.
Wakizungumza wakati wakipatiwa matibabu baadhi
ya majeruhi wa ajali hiyo wamesema kuwa ajali hiyo imesababishwa
na mwendo kasi wa mabasi hayo hatua ambayo ilisababisha kushindwa
kupishana katika daraja hilo hivyo kugongana uso kwa uso.
akizungumza kwa niaba ya mganga mkuu wa mkoa
wa Mara Dk Martin Khan,amesema kuwa wamepokea maiti na idadi kubwa ya
majeruhi na wengi wao hali zao si za kuridhisha.
Hata hivyo Dk Khan ametoa wito kwa wananchi
kujitokeza kujitolea damu kwani amesema kuwa hospital hiyo ya rufaa
ya mkoa wa mara inakabiliwa na upungufu mkubwa wa damu katika
kuhudimia wagonjwa wakiwemo majeruhi wa ajali.
kamanda wa polisi mkoa wa Mara ACP Alex Kalangi,
akizungumza na ITV kwa njia ya simu amethibitisha kutokea kwa ajali
hiyo na kwamba taarifa rasmi za jeshi la polisi zitatolewa baada ya
kupata taarifa kutoka kwa madaktari na kwamba ametoa wito kwa
wananchi kujitokea katika hospitali ya mkoa kwaajili ya kutambua miili
ya marehemu.